

18 March 2025, 14:34
Chuo cha Taifa cha usafirishaji NIT chatoa elimu ya usalama barabarani kwa wananchi mkoani Kigoma
Na Hagai Ruyagila
Chuo Cha taifa cha usafirishaji NIT kupitia kituo chake cha kikanda cha umahiri katika usalama barabarani kimeandaa mafunzo ya usalama barabarani kwa baadhi ya shule za Msingi halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma ili kuwasiaidi wanafunzi kufuata sheria za usalama barabarani na kupunguza ajali zinazoweza kuepukika.
Katika kuendelea kutoa mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi ambazo zipo kando ya barabara Mkuu wa kituo cha kikanda cha umahiri katika usalama barabarani (NIT) kanda ya Afrika mashariki na kusini mwa Afrika Godlisten Msumanje amesema lengo la mafunzo hayo ni kupunguza ajali kwa watembea kwa miguu pamoja na watumiaji wa vyombo vya moto.
Sauti ya mkuu wa kituo cha kikanda cha umahiri kanda ya Afrika mashariki na kusini mwa Afrika Godlisten Msumanje
Aidha Msumanje amesema ni muhimu madereva kuepuka kutumia vilevi wanapokuwa katika safari zao ili kupunguza ajali zinazoweza kuepukika.
Sauti ya Godlisten Msumanje
Copro Emmanuel Fussy kutoka jeshi la polisi kitengo cha dawati la elimu ya usalama barabarani wilaya ya Kasulu amesema wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za kuhakikisha wanapunguza ajali kwa watoto na wanafunzi wanapohitaji kuvuka barabara.
Sauti ya Copro Emmanuel fussy kutoka jeshi la polisi kitengo cha dawati la elimu ya usalama barabarani wilaya ya Kasulu
Baadhi ya wanafunzi kutoka shule ya mbalimbali za msingi halmashauri ya mji kasulu wamesema mafunzo hayo yamewasaidia kutambua umuhimu wa matumizi ya alama za barabarani.
Sauti za baadhi ya wanafunzi waliopata mafunzo
Katika halmashauri ya mji Kasulu Shule za msingi Kalema, Umoja, Murubona, Kiganamo na Kimobwa ni miongoni mwa shule ambazo zimenufaika na mafunzo hayo kwa siku ya kwanza.