Joy FM

Wakimbizi waishio kambi ya Nduta watakiwa kurejea nchini kwao

30 January 2025, 12:53

Wakimbizi wa kambi ya Nduta wakiwa katika mkutano ya uhamasishaji wa kurejea nchi Burundi, Picha na Lucas Hoha

Serikali imewataka wakimbizi kutoka nchini Burundi ambao wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi Nduta kurejea nchini kwao kwani kwa sasa usalama wa nchi hiyo umekwisha imarika.

Na Lucas Hoha

Wakimbizi  wanaohifadhiwa kwenye kambi ya wakimbizi Nduta iliyopo Wilaya ya Kibondo wamekubali kujiandikisha na kurejea  nchini  mwao mara baada ya Wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania na mashirika ya kimataifa yanayohudumia wakimbizi kuwahakikishia kuwa burundi ni salama.

Wakimbizi wa kambi ya Nduta wakiwa katika mkutano ya uhamasishaji wa kurejea nchi Burundi, Picha na Lucas Hoha

Wakizungumza na  waandishi wa habari baadhi ya wakimbizi hao wamesema wamepokea kwa mikono miwili ujumbe wa kuwataka kurudi kwao ili wasaidie kuleta maendeleo ya nchi yao, huku wakitoa wito kwa wakimbizi wenzao kukubali kurudi kwao.

Awali akitoa ujumbe wa kuwataka kurudi nchini Mwao Mkurugenzi wa idara ya huduma kwa wakimbizi kutoka Wizara ya mambo ya ndani nchini Sudi Mwakibasi amesema Kuna kila sababu za wakimbizi kurudi kwao na kuwa serikali ya Burundi imekubali kuwapokea watu wake.

Sauti ya Mkurugenzi wa idara ya huduma kwa wakimbizi Sudi Mwakibasi

Kwa upande wao, baadhi ya viongozi wanaohudumia wakimbizi akiwemo mratibu wa idara ya wakimbizi Kanda ya Kigoma John Mwita na wawakilishi wa UNHCR wametoa wito wa wakimbizi hao kuwa wanapoendelea kukaa kambini hapo wanapoteza vitu mhimu katika maisha yao ikiwemo kushindwa kujikwamua kiuchumi

Sauti za viongozi

Wakimbizi kutoka Burundi wakipiga ngoma ya asali wakati Mkurugenzi wa huduma kwa wakimbizi alipotembelea kambi hiyo, Picha na Lucas Hoha