Joy FM

Chakula kwa wanafunzi shuleni kupunguza utapiamlo

15 August 2024, 09:42

Pichana ni wanafunzi wakiwa darasani wakimsikiliza mwalimu wao, Picha na Mtandao

Serikali wilayani Kibondo mkoani Kigoma imesema itaendelea kuhakikisha wananchi wanachangia chakula shuleni ili kusaidia kuongeza ufaulu lakini kudhibiti utapiamlo unaotokana na ukosefu wa lishe kwa watoto.

Na James Jovin – Kibondo

Wazazi na walezi wilayani Kibondo mkoani Kigoma wametakiwa kuongeza juhudu za kuchangia chakula kwa wanafunzi shuleni ili kupunguza idadi kubwa ya watoto wanaoshinda na njaa hali inayowaathiri kiafya na masomo kwa ujumla.

Katika taarifa iliyotolewa na afisa lishe wa wilaya ya Kibondo Bw. Tumaini Muna katika kikao kazi cha kujadili masuala ya lishe wanafunzi wanaopata chakula shuleni kwa mwaka ni asilimia 66 pekee hali ambayo inakwamisha juhudi za serikali katika  kumaliza magonjwa ikiwemo utapiamlo.

Sauti ya afisa lishe wa wilaya ya Kibondo bw. Tumaini Muna

Kwa upande wake afisa tarafa wa tarafa ya Kifura Bw. Shekarata Omary amesema kuwa lishe inapaswa kuwa ajenda ya kudumu katika vikao mbalimbali ikiwa ni sambamba na kuwahamasisha wazazi na walezi kuongeza bidii katika kuchangia chakula shuleni kwa ajili ya watoto wao.

Sauti ya afisa tarafa wa tarafa ya Kifura Bw. Shekarata Omary

Kwa upande wake Bw. Steven Janks akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji katika kikao hicho amewataka watendaji kutumia sheria ndogo zinazohusu masuala ya chakula shuleni ili kuongeza idadi ya Watoto wanaokula chakula shuleni na hivyo kupunguza magonjwa ikiwemo utapiamlo.

Sauti ya bw. Steven Janks akimwakilisha mkurugenzi mtendaji Kibondo

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Kanali Agrey Magwaza amewataka viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha wanabaini changamoto mbalimbali zinazopelekea wazazi kushindwa kuchangia chakula shuleni na kuzifanyia kazi ili kuweza kupunguza ama kumaliza kabisa tatizo hilo.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kibondo kanali Agrey Magwaza