Joy FM

Mwenyekiti UWT aingilia kati ukosefu wa maji Kigoma

19 July 2024, 13:40

Mwenyekiti wa Umoja Wa Wanawake Chama Cha Mapinduzi Ccm Taifa, Mary  Chatanda, Picha na Kadislaus Ezekiel

Mamlaka ya maji safi na usafii wa mazingira manispaa ya kigoma ujiji, imetakiwa kuhakikisha inajenga kituo kipya cha kusambaza maji kwa wananchi wa kata ya mji mdogo wa mwandiga katika halmashauri ya wilaya kigoma ili kuwasaidia wananchi kuepukana na matumizi ya maji yasiyokuwa safi na salama.

Na Kadislaus Ezekiel – Kigoma

Mwenyekiti wa Umoja Wa Wanawake Chama Cha Mapinduzi Ccm Taifa, Mary  Chatanda ameagiza Watendaji wa waserikali wa idara ya maji kusaidia utatuzi wa changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama katika kata ya Mwandiga Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma,  na kusisitiza taratibu za kuwajengea mradi wa maji zianze mara moja.

Bi. Chatanda amesem hayo wakati wa mkutano na wananchi wa kata ya Mwandiga ambao wamelalamikia ukosefu wa maji safi na salama kwa kukosa mradi wa kusambaza maji toshelevu kata hiyo.

Sauti ya mwenyekiti wa UWT, Marry Chatanda
Baadhi ya wananchi walojitokeza kuhudhuria mkutano wa Mwenyekiti wa UWT kigoma

Kwa upande wake, Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Manispaa ya Kigoma Ujiji, KUWASA  Poas Kilangi, amesema kuwa tayari ameomba Serikali kiasi cha Bilioni Mbili ambazo zitatumika kujenga mradi wa maji toshelevu ambao utaweza kufikisha maji kwa wananchi huku  Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli amesema, atahakikidha anafuatilia hatua zote, ili wananchi wa Mwandiga waweze kupata maji bila usumbufu.

Sauti ya Mkurugenzi wa KUWASA na Mkuu wa wilaya Kigoma

Aidha Mkuu wa wilaya kigoma amesema kuwa serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha wananchi wanafikiwa na huduma karibu za kijamii.