Joy FM

Wananchi walia na TANESCO kutopewa umeme

18 July 2024, 09:07

Wananchi wa kijiji cha bitale wilayani kigoma wakiwa kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na mbunge Assa Makanika, Picha na Hamis Ntelekwa

Mbunge wa jimbo la kigoma kaskazini Assa Makanika amelitaka shirika la umeme mkoani kigoma TANESCO kuhakikisha wanapeleka huduma ya umeme kwa wananchi wa vijiji ambavyo havijafikiwa na huduma hiyo hali inarudisha nyuma shughuli za maendeleo.

Na Kadislaus – Kigoma Dc

Wananchi katika vijiji vya kata ya Mkongoro Halmashauri Ya Wilaya Ya Kigoma Mkoani Kigoma, wamewatuhumu viongozi wa TANESCO wilayani humo, kuwachukulia fedha zao Ili kupatiwa UMEME wa REA, huku wakiwatelekeza bila huduma kutolewa, na wengine kuingia hasara ya kununua vifaa vya umeme wakiwa na uhakika wa kupata nishati hiyo.

Mbunge wa kigoma kaskazini Mh. Assa Makanika akiwa kwenye mkutano wa hadhara, Picha na Hamis Ntelekwa

Wakizungumza katika mkutano wa viongozi, wananchi na mbunge wa jimbo la kigoma kaskazini mheshimiwa assa makanika, ambapo wananchi wa kata ya mkongoro wamelalamikia baadhi ya viongozi wa tanesco kuwatoza fedha wananchi, ili kuletewa nishati ya umeme bila mfanikio.

Sauti ya Wananci wa vijiji vya mkungoro akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara

Jambo hilo linamfanya mbunge assa makanika, kumtaka mhandisi wa umeme wilaya ya kigoma josephu kanje na kutolea ufafanuzi.

Sauti ya mhandisi wa umeme wilaya ya kigoma josephu kanje

Aidha mbunge Assa Makanika, akatoa maelekezo ya jumla kuhakikisha tanesco wanachukua hatua za kuwapeleka umeme wananchi ambao hajanifaika na huduma hiyo.

Sauti ya mbunge Assa Makanika