Joy FM

Umeme wa gridi ya taifa kuifungua Kigoma

3 July 2024, 14:21

Mwonekano wa nguzo za umeme, Picha na Mtandao

Serikali ya mkoa wa Kigoma imesema dhamira ya serikali kuu ni kuona Kigoma inakuwa na umeme wa uhakika ili kuendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Na Sadiki Kibwana – Kigoma

Jumla ya shilingi bilioni 434 zilizotolewa na serikali zimetumika katika ujenzi wa miundombinu ya nishati ya  umeme wenye kilovati 400 ili kuondoa changamoto za upatikanaji wa umeme wa uhakika katika mkoa wa Kigoma.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye, wakati akizungumza  na Joy Fm na kueleza  miradi mbalimbali inayojengwa na serikali mkoani hapa.

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye

Mh. Andengenye amesema hayo yamefanyika ili kuutoa mkoa wa kigoma kwenye giza ambapo umeme huo unaotoka Nyakanazi mpaka Kidahwe unatarajiwa kupokelewa tarehe 30 mwezi huu huku  umeme wa kutoka Tabora kwenda Nguruka wenye kilovati 132 unatarajiwa kuongezeka kwenye gradi ya Taifa.  

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye

Wakati huo huo, Mhe Andengenye amesema Benki ya dunia imetoa mkopo kwa Tanzania ili kigoma iweze kuzalisha umeme katika kijiji cha Igamba kutoka mto malagarasi ambapo mradi huo utazalisha megawati 49.9 ambazo zitaingia katika gradi ya taifa na kuongeza upatikanaji wa umeme.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye

Katika hatua nyingine Mhe. Andengenye amesema upatikanaji wa Nishati ya umeme utasaidia mkoa wa kigoma kufungua fursa mbalimbali ikiwemo maendeleo ya kibiashara na viwanda.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye