Joy FM

Wananchi Kasulu walia mabomba kutoa maji machafu

2 July 2024, 10:42

Diwani wa kata ya Kumunyika Seleman Kwirusha akiwa katika mkutano wa hadhara. Picha na Emmanuel Kamangu

Wananchi wa kata ya Kumunyika wamelalamikia serikali kupitia mamlaka ya maji Kasulu kuruhusu mabomba ya ya maji kuwa na tope hali inayoweza kusababisha magonjwa ikiwemo kuhara.

N a Emmanuel Kamangu – Kasulu

Diwani wa kata ya Kumunyika Bw. Selaman Kwirusha amemwagiza Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira katika mji wa Kasulu KUWASA kushughulikia kwa wakati  kero ya baadhi ya wananchi  wa kata ya Kumunyika kukabiliwa na utumiaji wa maji machafu yanayotoka katika mabomba.

Katika mkutano huo  ambao umeandaliwa na Diwani wa  kata ya Kumunyika Bw. Kwirusha wananchi wa  kata hiyo  wakaibua kero  mbalimbali ikiwemo kukabiliwa  na utumiaji wa  maji  machafu  yanayotoka  katika mabomba  ambapo wamedai wamekuwa  wakiugua minyoo na magonjwa ya kuhara na kufuatia changamoto hiyo kaimu mkurugenzi wa KUWASA Bw. Guttu Bundara akayatolea ufafanuzi.

Sauti ya wananchi wa kumunyika na kaimu meneja wa KUWASA

Aidha Diwani wa kata ya Kumunyika Bw, Seleman Kwirusha ameeleza mafanikio ambayo wamefanikiwa katika kata hiyo yenye mitaa mitano ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule  ya sekondari na msingi sambamba na uwepo wa barabra ya kuwaunganisha wananchi wa kata ya Kumunyika pamoja na wananchi wa kata ya Mhunga.

Sauti ya Diwani wa kata ya Kumunyika Bw, Seleman Kwirusha

Hata hivyo wanyeviti wa mitaa katika kata ya Kumunyika wametumia fursa ya mkutano huo wa hadhara kuwaaga wananchi wao huku wakiwaomba waendelee kuwaunga mkono katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa ili waendelee kuwawakilisha.