Joy FM

Walimu waaswa kutofanya kazi kwa mazoea

27 June 2024, 09:00

Pichani ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi upande wa Elimu Charles Msonde

Halmashauri ya wilaya Kibondo imetakiwa kutatua mahitaji ya walimu na kuacha kutumia lugha zisizo rafiki kwa walimu wanapopeleka changamoto zao  ili zitatuliwe.

Na James Jovin – Kibondo

Katika kurekebisha upatikanaji wa elimu bora hapa nchini walimu wilayani Kibondo  wameaswa kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea  ili kufikia malengo ya serikali na kuwapatia Watoto ujuzi utakaowasaidia katika Maisha

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi upande wa Elimu Charles Msonde alipokuwa akizungumza na Walimu wa shule za Msingi na sekondari wilayani Kibondo Mkoani Kigoma ambapo amesema Mkoa huo uko kiwango cha chini kielimu kutokana na ufundishaji usiozingatia vigezo.

Sauti ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi upande wa Elimu Charles Msonde

Amesema kila mwalimu anatakiwa kujipima utendaji wake wa kazi kwa kuwasaidia wanafunzi na kuwataka kuacha mazoea kazini.

Sauti ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi upande wa Elimu Charles Msonde

Baadhi ya walimu walioshiriki kikao hicho wamekili uwepo wa utendaji usioridhisha na baada ya kupata maelekezo wameahidi kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Sauti ya walimu wilayani kibondo

Pamoja na mambo mengine Msonde ameitaka halmashauri ya kibondo kutatua mahitaji ya walimu na kuacha kutumia lugha zisizo rafiki walimu wanapopeleka changamoto zao  ilizitatuliwe