Joy FM

Waislamu wametakiwa kuwajali wasiojiweza

17 June 2024, 15:34

Ni waumini wa dini ya kiislamu wilayani kasulu wakiwa katika swala ya Eid El Hajj, Picha na Hagai Ruyagila

Wakati waislamu duniani kote wakiwa wameungana kusherekea siku ya Eid El Hajj wito umetolewa kwao kuendelea kuwasaidia watu wasiojiweza hasa wanaishikatika mazingira magumu.

Na Hagai Ruyagila – Kasulu

Waumini wa dini ya Kiislamu wilayani Kasulu mkoani Kigoma wameaswa kusherehekea sikukuu ya Eid El Hajj kwa amani, uturivu na kuwajali wasiokuwa na uwezo kwa kuwapatia sadaka

Waislamu kote nchi wameungana kuadhimisha sikukuu ya Eid ambapo sala zimefanyika katika maeneo mbalimbali radio joy fm imefika katika msikiti wa ijumaa wa BAKWATA Kasulu mji na kuzungumza na shekhe mkuu wa wilaya hiyo Shekhe Masoud Swedi Kikoba ambaye amewasisitiza waumini hao kusherehekea kwa amani na pasipokutenda matendo maovu.

Shekhe mkuu wa wilaya hiyo Shekhe Masoud Swedi Kikoba, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya shekhe mkuu wa wilaya hiyo Shekhe Masoud Swedi Kikoba

Aidha Shekhe Kikoba ametoa wito kwa viongozi wa serikali kufanya kazi zao kwa uadilifu ili kuleta maendeleo katika taifa hili la Tanzania.

Sauti ya shekhe mkuu wa wilaya hiyo Shekhe Masoud Swedi Kikoba

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye amewaomba wanananchi kuendelea kuiombea serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  inayoongozwa na rais Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wake katika shughuli za kuwaletea maendeleo.

Sauti ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye

Nao baadhi waumini wa dini ya kiislamu Wilayani Kasulu wamesema ni jukumu lao kuilinda amani na kuendelea kusaidiana wao kwa wao.

Sauti ya baadhi waumini wa dini ya kiislamu Wilayani Kasulu
Baadhi waumini wa dini ya kiislamu Wilayani Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila