Joy FM

Usafirishaji holela wa kemikali ziwa Tanganyika hatari kwa viumbe

14 June 2024, 09:13

Picha ya samaki wakiwa wamekufa kwa kile kinachodaiwa kuvuta hewa ya kemikali, Picha na Mtandao

Serikali ya Tanzania imesema itaendelea kutoa elimu ya usafirishaji wa kemikali kupitia ziwa Tanganyika ili kusaidia kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza iwapo wasafirishaji hawatazingatia usafirishaji bora wa kemikali.

Na Kadilsaus Ezekiel – Kigoma

Wasafirishaji wa Bidhaa mbalimbali katika nchi jirani za Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, kupitia ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, wameomba Serikali kudhitibi usafirishaji holela wa kemikali kunusuru milipuko ambayo inaweza kusababisha madhara na hasara ikiwemo kuhatarisha uhai wa binadamu.

Baadhi ya wadau wa usafirishaji mkoani kigoma, wamesema ukosefu wa elimu ya utambuzi wa kemikali huenda ikasababisha milipuko wakiwa kazini, kutokana na uwepo wa madini yanayosafirishwa kutoka  nchi jirani, na kuingizwa mkoani Kigoma.

Picha ya wavuvi wakiwa wamevua samaki kwa kutumia kemikali, Picha na mtandao

“wengi wetu hatuna elimu ya masualaya kemikali kwahiyo unakuta tunasafirisha kwa kutumia uzoefu tu na pia inategemea na aina gani ya madini unayotakakusafirisha na hasa carboni ndio tumekuwa tukisafirisha”

Sauti ya wadau wa usafirishaji wa kemiakali ziwa tanganyika

Kwa upande wake meneja wa Bandari za ziwa tanganyika davis mabula amesema kemikali nyingi zinazosafirishwa zinatokea nchi jirani ya Congo na wamekuwa wakidhiti kwa kufanya ukaguzi, huku mkurugenzi wa huduma za udhibiti mamlaka ya  kemikali serikalini daniel dio akihakikisha usalama kwa kuendelea kuelimisha jamii.

Sauti ya meneja wa bandari za ziwa tanganyika

Aidha mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Kigoma mheshimiwa Thobias Andengenye, afisa biashara mkoa wa kigoma Deograius Sangu, amesema kutokana na kemikali hizo kuathili jamii ni wajibu sheria zifuatwe kulinda rasrimali watu.

Afisa biashara mkoa wa kigoma Deograius Sangu, Picha na Emmauel Kamangu
Sauti ya Afisa biashara mkoa wa kigoma