Joy FM

“DC kibondo wanawake wanafanyiwa ukatilii hawasemi”

12 June 2024, 12:09

Baadhi ya viongozi wa kata na viongozi wa KIPAFO wakiwa katika kikao cha uzinduzi wa mradi wa MWANAMKE SIMAMA, Picha na James Jovin

Katika kukabiliana na vitendo vya ukatilii na unyanyasaji kwa wanawake na watoto, wadau na serikali wametakiwa kuungana kwa pamoja kushughulikia ukitilii dhidi ya vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikiacha kovu na huzuni miongoni mwa wahanga wa matukio hayo.

Na James Jovin – Kibondo

Shirika lisilo la kiserikali Kibondo Paralegal Foundation (KIPAFO)  wamezindua mradi wa majaribio MWANAMKE SALAMA wenye dhumuni kupambana na  ukatili wa kijinsia katika wilaya ya Kibondo na kuongeza juhudi za kutetea haki za wanawake na kukuza utu wao katika jamii.

Hayo yamebainishwa na mratibu wa mradi huo kutoka shirika la KIPAFO bw. Mussa Mashishanga wakati wa uzinduzi wa mradi huo mbele ya mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Agrey Magwaza  na wadau wa mradi huo

Bw. Mashishanga amesema kuwa mradi huo utatekelezwa katika kata tano ndani ya wilaya ya Kibondo na kushughulikia ukubwa wa matatizo, matokeo na changamoto zinazohusiana na unyanyasaji wa kijinsia.

Sauti ya mratibu wa mradi huo kutoka shirika la KIPAFO bw. Mussa Mashishanga

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa shirika la KIPAFO wilayani Kibondo bw. Japhet Razalo amewataka viongozi katika kata zilizochaguliwa wakiwemo madiwani na watendaji kutoa ushirikiano katika shughuli hiyo ili kusaidia kutatua changamoto za ukatili wa kijinsia hasa kwa wanawake na wasichana.

Sauti ya Mkurugenzi wa shirika la KIPAFO wilayani Kibondo bw. Japhet Razalo

Naye Mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Agrey Magwaza amewataka wadau wote wa mradi wa Mwanamke salama wakiwemo viongozi wa dini kuwa vinara wa kupinga ukatili wa kijinsia hali itakayosaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza tatizo hilo ndani ya jamii.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Agrey Magwaza