Joy FM

“Wakulima tumieni mbegu bora za kahawa”

10 June 2024, 10:48

Miche wa kawaha ikiwa tayari kwa ajili ya kupandwa, Picha na Michael Mpunije

Serikali wilayani Kasulu mkoani Kigoma inatarajia kugawa mbegu bora za kahawa kwa wakulima ili waweze kulima kilimo chenye tija ambacho kitakuwa na mazao ya kutosha na yenye ushindani kwenye soko la ndani na nje ya nchi.

Na Michael Mpunije

Wakulima wa zao la kahawa wilayani Kasulu mkoani kigoma wametakiwa kufuata hatua bora za kilimo hicho kwa kutumia miche bora yenye uwezo wakukabiliana na magonjwa yanayo shambulia zao hilo  ili kuleta ufanisi kupitia kilimo hicho.

Hayo yamejiri katika kikao kuwajengea uwezo wa kulima wa zao la kahawa na maafisa ugani kutoka halmashauri ya mji kasulu na halmshauri ya wilaya ya Kasulu ambapo kilimo hicho kinatajwa kuleta  tija kwa wakulima wazao hilo ikiwa watazingatia hatua bora za kilimo.

Mkulima wa zao la kahawa akiwa anavuna kahawa, Picha na Mtandao

Akizungumza mara baada ya kutamatika kwa mafunzo hayo yaliyodumu kwa siku mbili kiongozi kutoka kituo kidogo cha utafiti wa kahawa Tacri mwayaya bi Sophia malinga amewataka wakulima  kuacha kilimo cha mazoea ambacho kimekuwa kikichelewesha mafanikio yao.

Sauti ya kiongozi wa kituo cha utafiti wa kahawa TACRI Mwayaya

Baadhi ya wakulima viongozi ambao wameshiriki katika mafunzo hayo Yosamu zefania na Aneth ntamsano wamesema watahakikisha wanatoa Elimu kwa wakulima wengine ili kuleta matokeo chanya ambayo yatasaidia kukuza uchumi wao huku wakiomba kuwepo soko la uhakika la zao hilo.

Sauti ya wakulima wa kahawa kasulu

Mratibu wa kahawa katika halmashauri ya mji kasulu bw Eliakimu john amesema wamezalisha zaidi ya miche milioni 1 ambayo wanatarajia kuigawa kwa wananchi mapema mwezio oktoba wakati wa maandalizi ya kilimo.

Mratibu wa zao la kahawa wilayani kasulu