Joy FM

Bidhaa zateketea kwa moto, maduka 12 yakinusurika Kasulu

5 June 2024, 13:15

Afisa wa jeshi la zimamoto akiwa katika duka lililoteketeka kwa moto, Picha na Hagai Ruyagila

Wananch wilayani kasulu mkoani kigoma kuendelea kuchukua tahadhari za majanga ya moto ili kuepuka hasa zinazojitokeza baada ya kutokea majanga ya moto.

Na Hagai Ruyagila – Kasulu

Duka moja limeungua kwa moto katika soko kuu la Kasulu Mjini lililopo jirani na eneo la round about kata ya Kumsenga halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma likiwa na bidhaa ya mabegi huku zaidi ya maduka 12 yakinusurika kuungua kwa Moto.

Ni Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo akiwemo Boaz Saigoni, Dunia Ndebheimana, Elibariki Alex na Enos Kaele wameeleza kile walichokiona kuwa ni chanzo cha duka hilo kuwaka moto.

Sauti za mashuhuda wa tukio la moto kasulu.

Kwa upande wake Mmiliki wa duka hilo ambalo limewaka moto Bw, Danfrod John amelishukuru Jeshi la zimamoto na uokoaji pamoja na baadhi ya wananchi kwa kuokoa baadhi ya bidhaa zilizokuwa ndani ya duka hilo sambamba na kubainisha thamani ya vitu vilivyoungua.

Mmiliki wa duka lililoteketea kwa moto wilayani kasulu, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya mmiliki wa duka lililoteketea kwa moto kasulu

Naye Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Kasulu Inspector Anthony Marwa amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wafanyabiashara kuwa na vifaa kinga vya moto pamoja na kutoa taarifa za haraka pindi majanga ya moto yanapotokea.

Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Kasulu Inspector Anthony Marwa, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Kasulu Inspector Anthony Marwa