Joy FM
Joy FM
13 February 2026, 10:05

Watoto yatima ni sehemu muhimu ya jamii yetu na hawa ni watoto waliopoteza wazazi wao au walezi wao, hivyo hukosa malezi, ulinzi na msaada wa karibu wa kifamilia na kutokana na hali hiyo, watoto yatima hukumbana na changamoto nyingi kama ukosefu wa mahitaji ya msingi, elimu, na msaada wa kihisia.
Na Prisca Kizeba
Jamii Mkoani Kigoma imeaswa kuwasaidia watoto waliopo katika manzigira hatarishi hasa watoto yatima wanaoishi katika vituo vya kulea watoto.
Hayo yamesemwa na Mgurungenzi wa Kanda ya Manispaa ya Kigoma Mchungaji Kanoni Andasoni Bilasa wakati akigawa zawadi kwa watoto yatima katika kituo cha Matyazo kilichopo Kata ya Kalinzi Halmashauri ya Wilaya Kigoma na kuwa jamii inatakiwa kuwa na upendo na huruma katika kuwahudumia watoto yatima
Mchungaji Kanoni amezitaja zawadi hizo kuwa zimegharima shilingi milioni tatu laki tatu na mia tano na wameguswa kama kanisa la Anglikana Kanda ya Manisapaa kwa kuwatembelea watoto hao.

Akipokea zawadi hizo, Mwangalizi na mlezi wa watoto hao Bi. Ziada Yasin ameshukuru kanisa la Anglikani Kanda ya Manisapa na kuwa zawadi walizotoa zimegusa moja kwa moja mahitaji ya watoto na kuomba tasisi zingine kuendelea kuwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu
Nao baadhi ya viongozi wa kanisa hilo akiwemo mwenyekiti wa msafara huo Fanuel Magambo na Mama Mkurugennzi wa kanda hiyo Dorcas Bilasa wameeleza namna gani wamekuwa na msukumo wa kuwatembelea watoto hao.