Joy FM

Zaidi ya wahamiaji 1200 waliingia Kigoma kinyume cha sheria

4 February 2026, 13:15

Wananchi wa Kijiji cha Kaseke wakiwa kwenye mkutano wa hadhara uliitisha na uhamiaji, Picha na Sadiki Kibwana

Idara ya uhamiaji Mkoani Kigoma imeendelea na kampeni ya mjue jirani yako inayolenga kuwatambua wahamiaji haramu wanaoingia nchini kinyume cha sheria.

Na Sadick Kibwana

Zaidi ya wahamiaji haramu elfu moja na mia mbili kutoka nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameingia nchini pasipo kufata sheria kupitia vipenyo vya mipakani vilivyopo mkoa wa Kigoma kuanzia Desemba 2025 na Januari mwaka huu jambo ambalo linahatarisha usalama wa nchi.

Hayo yamesemwa katika mkutano na wananchi uliofanyika kijiji cha Kaseke, Kata ya simbo Halmashauri ya Wilaya Kigoma Mkoa wa Kigoma na Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa Mrakibu Mwandamizi Dominick Kibuga.

Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa Mrakibu Mwandamizi Dominick Kibuga, Picha na Sadiki Kibwana

Mrakibu Mwandamizi Kibuga amesema idadi ya wanao vuka mipaka bila utaratibu inaendelea kuongezeka hivyo ipo haja ya wananchi kulijua hilo.

Sauti ya Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa Mrakibu Mwandamizi Dominick Kibuga

Mwenyekiti msaidizi wa Kijiji cha Kaseka, Bwana Denis Nyarusage amesema elimu hiyo inapaswa kutolewa mara kwa mara ili ifahamike zaidi.

Sauti ya Mwenyekiti msaidizi wa Kijiji cha Kaseka, Bwana Denis Nyarusage

Nao baadhi ya Wananchi wameshukuru idara ya Uhamiaji kwa kuwapatia elimu juu ya suala la kuwa na wahamiaji.

Sauti ya baadhi ya Wananchi

Elimu iliyotolewa na Ofisi ya Uhamiaji mkoa wa Kigoma ni mwendelezo wa elimu kwa umma kutolewa ambapo mpaka sasa zaidi ya Vijiji vi4 vimeshafikiwa na kupatiwa elimu hiyo.

Wananchi wa Kijiji cha Kaseke wakiwa kwenye mkutano wa hadhara uliitisha na uhamiaji, Picha na Sadiki Kibwana