Joy FM

Wananchi watakiwa kutoa taarifa za wahamiaji haramu Kigoma

21 January 2026, 14:28

Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma, Dominick Emmanuel Kibuga akiwa na maafisa wa Polisi wakiwa kwenye mkutano, Picha na Sadiki Kibwan

Idara ya uhamiaji Mkoani Kigomma imeendelea na kampeni ya mjue jirani yako yenye lengo la kuwabaini wahamiaji haramu wanaoishi nchini kinyume cha sheria

Na Sadick Kibwana

Wananchi wametakiwa kutoa taarifa za uwepo wa wahamiaji wanaoishi maeneo yao kinyume na sheria  za nchi ili raia waweze kufanya shughuli za maendeleo kwa amani na usalama.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma, Dominick Emmanuel Kibuga katika mkutano na wananchi uliyofanyika Kata ya Bitale wilaya ya Kigoma ulioenda sambamba na kaulimbiu inayosema mjue jirani yako.

Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma, Dominick Emmanuel Kibuga, Picha na Sadiki Kibwana

Amesema usalama wa wilaya ni jukumu la kila raia hasa linapokuja suala la wageni kuingia nchini kinyemela ambao wengi wao hujihusisha na matendo ya uhalifu.

Carson Mzava kutoka Ofisi ya Upelelezi Mkoa amesema kuwepo kwa wahamiaji haramu kumechangia wimbi la uhalifu kuongezeka hivyo ni muhimu kutoa taarifa.

Baadhi ya wananchi walihudhuria mkutano huo wamesema elimu hiyo itolewe mara kwa mara ili jamii  iwe na ufahamu.

Baadhi ya wananchi walihudhuria mkutano huo, Picha na Sadiki Kibwana

Wilaya ya Kigoma inazungukwa na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hali inatajwa zaidi ya wahamiaji haramu elfu 4 huvuka mipaka na kuingia nchini na kufanya shughuli za kiuchumi bila kufata utaratibu.