Joy FM

Ujumbe wa viongozi Congo watoa msaada kwa wakimbizi Kigoma

15 January 2026, 11:04

Wakimbizi wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi waliotembelea Camp ya wakimbizi waliopo Kibirizi, Picha na Orida Sayon

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, Barbara Dotse amesema shirika hilo linaendelea kutafuta fedha ili huduma za kibinadamu kwa wakimbizi hao wa Congo ziweze kurejea kawaida huku wakitafuta suluhisho la kudumu la wakimbizi hao kurejea nchini mwao.

Na Orida Sayon

Ujumbe wa viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imetembelea Kambi ya kuwapokea wakimbizi iliyoko Kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma ujiji na kutoa msaada wa vitu mbalimbali pamoja na chakula.

Ziara hiyo ni mwendelezo wa ziara ya kutembelea wakimbizi kutoka nchini Congo walioko katika kambi za wakimbizi Mkoani Kigoma ikiongozwa na Waziri anayeshughulikia masuala ya ustawi wa jamii, hatua za kibinadamu na mshikamano Eve Masudi .

Baadhi ya viongozi wa ujumbe huo wakikabidhi misaada kwa wakimbizi Camp ya Kibirizi, Picha na Orida Sayon

Mhe. Eve Masudi ametumia ziara hiyo kuishukuru shirika la umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR kwa kuwatunza wakimbizi na kumpongeza Rais wa Tanzania kuwa kiongozi bora mwanamke na mfano wa kuigwa na wanawake viongozi Afrika.

Sauti ya waziri anayeshughulikia masuala ya ustawi wa jamii, hatua za kibinadamu na mshikamano Eve Masudi

Akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Tanzania,  Naibu Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Millya amesema Tanzania inajali wakimbizi waliokimbia hali ya vurugu nchini kongo na inaendelea kuiombea ili iweze kurejea katika amani.

Sauti ya Naibu Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Millya
Baadhi ya viongozi wakiwa wamewasili katika Camp ya Kibirizi kutembelea wakimbizi wanaohifadhiwa kituoni hapo, Picha na Orida Sayon

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkaazi wa shirika la umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR Tanzania Bi. Barbra Dotse ameishukuru Tanzania na Congo kwa ushirikiano wanatoa kwa shirika hilo hasa kuwajali wakimbizi.

Sauti ya Mwakilishi Mkaazi wa shirika la umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR Tanzania Bi. Barabra Dotse

Baadhi ya wakimbizi wakawa na haya ya kueleza kwa viongozi wao toka kongo na Tanzania.

Sauti ya wakimbiza