Joy FM

Umoja wa wanaume watoa msaada kambi ya wazee Kigoma

19 November 2025, 12:22

baadhi ya wazee wakipokea msaada wa vitu mbalimbali kutoka kwa umoja wa majirani wanaume waishio Kata ya Kibirizi  Mtaa wa Buronge

Na Lucas Hoha

Kikundi cha umoja wa majirani wanaume waishio Kata ya Kibirizi  Mtaa wa Buronge Manispaa ya Kigoma Ujiji wametoa msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha kulelea wazee wasiojiweza cha Silabu lengo likiwa ni kuonesha umoja katika kuisaidia jamii ya watu wenye mahitaji.

Wakikabidhi msaada  huo baadhi ya viongozi wa kikundi hicho akiwemo Zabron Yusufu  na Octavian Lutasha wamesema wamedhamiria kufanya shughuli za kijamii na kuyafikia makundi mbalimbali yenye uhitaji wakiwemo yatima, wazee na wagonjwa.

Sauti ya wanakikundi

Awali akipokea msaada huo, Afisa ustawi wa jamii katika makazi ya wazee wasiojiweza Fred David pamoja na mambo mengine amesema wazee hao wanamahitaji ya vitu mbalimbali ambapo ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia

Afisa ustawi

Baadhi ya wazee wanaolelewa katika kituo hicho, wameshukuru kikundi cha umoja wa majirani wanaume wa  Buronge kuwapatia msaada huo, huku wakitaja baadhi ya mahitaj yao ambayo wangependa jamii iwasaidie ikiwemo mavazi na chakula.

wazee