Joy FM
Joy FM
23 October 2025, 15:30

Watu wenye ulemavu wameomba jamii kutoendelea kuwanyanyapaa badala yake wawaelekeze na kuwasaidia ili nao waweze kufanya shughuli za kuwaingizia kipato na kuchangia pato la familia na Taifa
Na Mwandishi wetu
Mgombea ubunge Jimbo la Kigoma kusini Nuru Kashakali maarufu Kandahari ameahidi kuona uwezakano wa kuanzisha mfuko rasmi wa kusaidia na kuwezesha watu wenye ulemavu katika jimbo hilo kiuchumi.
Kauli ya Mgombea huyo ameitoa akiwa Kijiji cha Uvinza katika mkutano wa kampeni kufuatia mmoja wa walemavu Aziz Ally kuomba msaada akilalamika jamii ya walemavu kutengwa nakunyanyapaliwa kiuchumi.

Kandahari amesisitiza kuwa walemavu wakiwezeshwa wanaweza kuzalisha mali na kumudu maisha yao na kuongeza pato kwa nchi badala ya kutelekezwa na kubaki kuwa omba omba.
Kandali amesisitiza kuwa adhima yake kubwa ni kuwasaidia walemavu kuishi maisha ya staha kama ambavyo amepanga kutoa mikopo kwa makundi mengine ya vijana na akina mama nakwamba yote atatekeleza mara atakaposhinda kiti cha Ubunge.
Kandahari alifanya mikutano mingine eneo la Kata ya Basanza, kata ya Uvinza katika vijiji vya Chakulu na Lugufu Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma
