Joy FM

Tanzania na UNHCR kufuta hadhi ya ukimbizi kwa wakimbizi wa Burundi

16 October 2025, 23:33

Baadhi ya viongozi waliohudhuria mkutano wa kuhamasisha wakimbizi wa Burundi kurudi kwao, Picha na Tryphone Odace

Licha ya Serikali na shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kuhamasisha wakimbizi waliopo katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu tangu mwaka 2017 na kuonekana zoezi la kurejea nchini kwao kwa hiari kusuasua sasa mwarobaini wa kuwarudisha wakimbizi hao ni pamoja na kuwafutia hadhi ya kuwa mkimbizi ili waweze kurejea nchini kwao kwani tayari Burundi ipo salama

Na Mwandishi wetu

Serikali ya Tanzania  na shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR zimetangaza kufuta hadhi ya ukimbizi kwa wakimbizi kutoka Nchini Burundi wanaoishi katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu iliyopo Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma kwani tayari muda wa kuishi nchini kama wakimbizi umeisha na hivyo hawana budi kuridi nchini kwao kutokana na usalama na amani uliopo nchini Burundi.

Wito huo umetolewa leo na Mkurugenzi wa huduma idara ya wakimbizi, Wizara ya mambo ya ndani ya nchi, Sudi Mwakibasi wakati akizungumza na wakimbizi hao ambapo mesema tayari uhamasisho wa wakimbizi kurudi kwao  umeshafanyika na hivyo hawana budi  kurudi na kwenda kuijenga nchi yao kwani imetulia na amani ya kutosha ili waweze kujiletea  maendeleo.

Sauti ya Mkurugenzi wa huduma kwa wakimbizi, Wizara ya mambo ya ndani
Mkurugenzi wa huduma kwa wakimbizi kutoka wizara ya mambo ya ndani ya Nchi Sudi Mwakibasi akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, Picha na Tryphone Odace

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amewataka wakimbizi hao waweze kurudi kwao ili wakaendelee na shughuli za kiuchumi katika taifa lao kwani kuendelea kuishi kambini kunawafanya watoto na vijana kukosa huduma muhimu na kupoteza malengo yao ya nchi yao.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro

Mwakilishi mkazi wa shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Babra Dotse amesema kuwa kulingana na utafiti walioufanya wamebaini kuwa wakimbizi hawana budi kurudi kwao kwani tayari kuna amani ya kutisha licha ya kuwa wengi wao wanaonyesha kuhitaji kwenda nchi ya tatu.

Mwakilishi Mkazi wa UNHCR hapa Nchini akizungumza wakati wa kuhamasisha wakimbizi wa Burundi kurudi kwao, Picha na Tryphone Odace
Sauti ya Mwakilishi Mkazi wa UNHCR hapa Nchini Tanzania

Naye balozi wa Burundi katika  ubalozi mdogo wa Kigoma Kekenwa Jeremiah amewaasa wakimbizi kutoka Burundi waweze kurejea nyumbani kwao kwani  machafuko yaliyosababisha wakimbie nchi yao yameshaisha baada ya makubaliano ya mkataba wa kumaliza tofauti kati ya makundi yaliyokuwa yakihasiamiana na sasa umoja na mshikamano upo vizuri nchini humo.

Wakimbi kutoka Burundi wakiwa katika mkutano wa kuhamasishwa kurudi kwao, Picha na Tryphone Odace
Sauti ya balozi wa Burundi katika  ubalozi mdogo wa Kigoma Kekenwa Jeremiah

Aidha Balozi Kekenwa amesema kuwa kwa sasa Burundi kuna amani ya kutosha na maendeleo yanaendelea kukua na kuongeza uchumi wa jamii yao na Taifa kwa ujumla.