Joy FM

Wagombea vyama vya siasa waonywa kutovunja amani Kasulu

11 September 2025, 13:39

Askofu wa Kanisa la FPCT Jimbo la Kasulu Shedrack Bunono, Picha na Hagai Ruyagila

Wito umetolewa kwa wagombea kuhakikisha wanafanya kampeni za ustaarabu na kuheshimu kanuni na sheria za Nchi ili kuepuka kusababisha vurugu kwa Taifa

Na Hagai Ruyagila

Wagombea wa nafasi mbali mbali za uongozi katika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, wameshauriwa kuhakikisha kampeni zao zinafanyika kwa amani, bustarabu na ustarabu ili kuendeleza utulivu uliopo Nchi.

Wito huo umetolewa na Askofu wa kanisa la FPCT Jimbo la Kasulu, Shedrack Bunono wakati akizungumza na viongozi wa serikali, viongozi wa dini na wa vyama vya siasa Mjini Kasulu.

Askofu Bunono amewasisitiza wanasiasa kutumia lugha ya staha na kuepuka maneno ya uchochezi ambayo yanaweza kusababisha migogoro au kuleta sintofahamu miongoni mwa wananchi.

Sauti ya Askofu wa kanisa la FPCT Jimbo la Kasulu, Shedrack Bunono

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa chama cha Wananchi CUF wilaya ya Kasulu Ndg. Vedasto Kagina ameeleza kuwa wamejipanga kuhakikisha wanafanya kampeni kwa ustarabu, kwa kufuata sheria na miongozo ya tume huru.

Sauti ya Mwenyekiti wa chama cha Wananchi CUF wilaya ya Kasulu Vedasto Kagina

Nao baadhi ya Wananchi wa wilaya ya Kasulu wameunga mkono kauli hizo na kuwataka wagombea wote kuzingatia sheria na taratibu za uchaguzi ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima.

Sauti ya baadhi ya Wananchi wa wilaya ya Kasulu

Wito huu unakuja katika kipindi ambacho nchi inajiandaa kuelekea uchaguzi mkuu, ambapo wadau mbalimbali wanaendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha amani, mshikamano na umoja wa taifa.

Viongozi wa serikali, dini na wa vyama vya siasa, Picha na Hagai Ruyagila