Joy FM

Zitto Kabwe autaka ubunge Kigoma Mjini

8 September 2025, 09:38

Wafuasi wa chama cha ACT Wazalendo wakiwa katika uwanja wa Mwami Ruyagwa kusikiliza sera za mgombea wao Zitto Kabwa, Picha na Tryphone Odace

Mgombea ubunge wa jimbo la Kigoma mjini kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amewataka wapiga kura katika jimbo hilo kumpa kura nyingi za ndiyo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu ili aweze kurudi bungeni kuwatumikia lakini pia kulinda heshima ya bunge hilo.

Na Tryphone Odace

Chama cha ACT Wazalendo  Jimbo  la Kigoma  Mjini  kimezindua  rasmi kampeni   zake za kuwania kutwaa  jimbo hilo na kufanya mkutano  wake wa kwanza  wa kumnadi  mgombea wake Zitto Zuberi Kabwe.

Akizungumza na mamia ya wafuasi wa chama hicho pamoja  na  wananchi  waliojitokeza katika uzinduzi wa kampeni  hizo katika viwanja vya Mwami Ruyagwa  vilivyopo kata ya Gungu Manispaa ya Kigoma Ujiji, mgombea ubunge wa ACT Wazalendo Jimbo la Kigoma Mjini Zitto  Kabwe, amewaomba wamtume tena bungeni akafanye kazi ya kuwawakilisha na kujenga heshima  ya watu wa Kigoma.

Mgombea ubunge wa ACT Wazalendo Jimbo la Kigoma Mjini Zitto  Kabwe
Mgombea ubunge kupitia ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiwasalimia wafuasi wa chama hicho mara baada ya kuwasili katika uwanja Mwami Ruyagwa Gungu, Picha na Tryphone Odace

Zitto amewataka wakazi wa jimbo la Kigoma  Mjini kutofanya makosa ya kuchagua mgombea wa chama  kingine, akisisitiza kuwa huu ni wakati ambao  jimbo hilo linahitaji kiongozi kama yeye ili kuendeleza  miradi iliyoanzishwa na chama  chake kilipoongoza halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kati ya mwaka 2015 na 2020.

Aidha Zitto Kabwe amewataka wapiga kura katika jimbo la Kigoma Mjini kutumia miezi hii miwili ya kampeni  kutafakari kwa kina aina ya kiongozi wanayemtaka ili kufanya uamuzi sahihi ifkapo Oktoba 29,2025.

Mgombea ubunge wa ACT Wazalendo Jimbo la Kigoma Mjini Zitto  Kabwe

Kwa upande wake, Mwenyekiti  wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo, amewataka vijana na wananchi wote wa jimbo la Kigoma Mjini, kumchagua Zitto Kabwe ili awawakilishe bungeni kwa sababu tayari ameonyesha kuwa ndiye anayeweza kufanya hivyo.

Sauti ya Mwenyekiti  wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo
Wafuasi wa chama cha ACT Wazalendo, Picha na Tryphone Odace