Joy FM

Askari wa jeshi la kiba watakiwa kuwa wazalendo Kigoma

27 August 2025, 16:36

Mkuu wa Wilaya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua akiwa na viongozi wa ulinzi, Picha na Hagai Ruyagila

Vijana waliohitimu mafunzo ya awali ya Jeshi la akiba wameaswa kuwa wazalendo

Na Lucas Hoha

Mkuu  wa Wilaya  ya Kigoma Dkt Rashird Chuachua amewataka vijana waliohitimu mafunzo ya awali ya jeshi la akiba kuwa wazalendo katika kulinda na kuhakikisha nchi yao inakuwa salama na kukataa maovu yanayofanywa watu wasio waaminifu.

Katika hafla ya kufunga mafunzo ya awali kwa wahitimu wa mafunzo ya jeshi la akiba ambayo yamefanyika katika uwanja wa lake Tanganyika uliopo Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt Rashid Chuachua pamoja na mambo mengine amewataka askari kuwa waaminifu katika kuwatumikia watanzania.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt Rashid Chuachua

Naye Katibu tarafa wa Kigoma kusini Dahaye Anney amewaomba vijana waliopo mtaani kujiunga na mafunzo ya jeshi la akiba.

Awali akisoma lisala kwa niaba ya wahitimu wa mafunzo Philipo James amesema  katika  mafunzo hayo wamejifunza vitu mbalimbali ikiwemo utiifu, huku wakiomba kupewa kipaumbele katika shughuli mbalimbali za serikali.

Msoma lisala

Mafunzo ya askari hao yamedumu kwa miezi 4 na kwa mjibu wa lisala jumla ya wahitimu 116 wamemaliza mafunzo hao.

Maaskari waliohitimu mafunzo ya awali ya jeshi la akiba, Picha na Lucas Hoha