Joy FM

Majambazi watatu wauawa Kigoma

5 August 2025, 13:08

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma Filemon Makungu, Picha na Kadislaus Ezekiel

Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma limethibitisha watu watatu wanaosadikiwa kuwa Majambazi kuuawa katika tukio la majibizano ya risasi katika jaribio la kutaka kuteka magari  eneo la Kumshindwi Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma Filemon Makungu amesema katika tukio hilo wamekamata silaha mbalimbali ikiwemo Bunduki moja aina ya  Ak 47, magazine moja , risasi kumi pamoja na silaha za jadi.

Kufuatia tukio hilo, wananchi wameomba Jeshi la Polisi kuongeza nguvu kudhibiti matukio ya ujambazi na kufanya mkoa wa Kigoma kuwa shwari bila hofu.

Miili ya watu waliouawa bado haijatambuliwa na hivyo kuhifadhiwa   katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo huku wengine waliokimbia katika tukio hilo wakiendelea kusakwa na Jeshi la Polisi.

Sauti ya Kadislaus Ezekiel Mwandishi Joy Fm