Joy FM

Wahamiaji haramu 926 wakamatwa Kigoma

8 July 2025, 16:11

Ni wahamiaji walikamatwa na idara ya uhamiaji Mkoani Kigoma, Picha na Lucas Hoha

Viongozi wa Serikali za mitaa na vijiji Mkoani Kigoma wametakiwa kufuatilia na kutoa taarifa za watu wanaoingia kwenye maeneo yao ili kujua kama ni wahamiaji haramu.

Na Lucas Hoha

Idara ya uhamiaji  Mkoa wa Kigoma kupitia  misako mbalimbali iliyofanyika June 2025 imefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 926 wakiwa na makosa mbalimbali ikiwemo baadhi yao kuingia nchini bila kufuata sheria ambapo raia 706 kati ya hao wanatoka katika nchi ya Burundi.

Hayo yamesemwa na Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma Dismas Mlula wakati akizungumza na waandishi wa habari ili kutoa taarifa ya mafanikio ya misako inayofanyika ya watu ambao wanaishi nchini kinyume na sheria.

Sauti ya Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma Dismas Mlula

Wakati huohuo, Mlula amewaomba raia wa kigeni wanaokuja nchini Tanzania kwa ajili utafutaji wa halali kufuata utaratibu wa kisheria kabla yakuingia nchini na kuwataka  wenyeviti wa Vijiji na watendaji wa kata kutoa tarifa kwa idara ya uhamiaji kuhusu wahamiaji haramu ili kulinda amani iliyopo.

Sauti ya Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma Dismas Mlula

Aidha Idara ya uhamiaji imekemea tabia ya baadhi ya raia wa Tanzania kujihusisha na usafirishaji wa binadamu kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine na kuwataka kuacha tabia hiyo.

Sauti ya Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma Dismas Mlula