Joy FM

Wakristo waaswa kushiriki na kuombea uchaguzi

18 June 2025, 15:36

Waumini wa kanisa Anglikana wakiwa katika ibaada, Picha na Hagai Ruyagila

Kuelekea uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi oktoba mwaka huu, Wakristo wametakiwa kuendelea kuombea amani na utulivu

Na Hagai Ruyagila

Waumini wa dini ya Kikristo wametakiwa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi pamoja na kuuombea uchaguzi huo ufanyike kwa amani na utulivu.

Wito huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika, Mhashamu Emmanuel Bwatta, wakati wa ibada maalum ya Sakramenti ya Kipaimara na uwekaji wa jiwe la msingi kwenye jengo jipya la Kanisa la Anglikana Murusi, linaloendelea kujengwa kwa ajili ya ibada.

Sauti ya Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika, Mhashamu Emmanuel Bwatta
Askofu Emmanuel Bwatta wa DWT Kasulu akiwa na Askofu Rachel Treweek kutoka Dayosisi ya Gloucester ya Nchini Uingereza, Picha na Hagai Ruyagila

Askofu Bwatta amesema ni jukumu la kila muumini kuombea uchaguzi huo ili ufanyike kwa amani, lakini pia kwa wale wanaohisi kuitwa na Mungu kuongoza, wachukue hatua ya kuchukua fomu na kugombea nafasi za uongozi kwa ajili ya kuliletea taifa maendeleo na kudumisha maadili.

Sauti ya Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika, Mhashamu Emmanuel Bwatta

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Kasulu Mjini, Mchungaji Canon Laurent Magogwa, ameeleza umuhimu wa uchaguzi huo na kuwasihi kuchagua viongozi bora.

Sauti ya Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Kasulu Mjini, Mchungaji Canon Laurent Magogwa

Baadhi ya waumini wamesema wana matumaini kuwa uchaguzi huo utafanyika kwa amani, huku wakitoa maoni tofauti kuhusu ushiriki wao katika siasa na mchakato wa uchaguzi.

Sauti ya Baadhi ya waumini

Ibada hiyo ya kipekee imehudhuriwa na waumini kutoka maeneo mbalimbali ya Kasulu na wageni wengine kutoka nchini Marekani na Uingereza ikiwa ni ishara ya mshikamano na umoja wa kiroho.