Joy FM

Askofu Joseph Mlola ahimiza amani, kuliombea Taifa

12 May 2025, 12:54

Askofu wa Jimbo katoliki la Kigoma Muhashamu askofu Joseph Roman Mlola, Picha na Tryphone Odace

Viongozi wa dini na jamii wameaswa kuliombea Taifa dhidi ya matukio yanaendelea kwenye jamii ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa amani.

Na Tryphone Odace

Askofu wa Jimbo Katoliki la Kigoma Joseph Mlola amewataka waumini wa kanisa hilo na watanzania kwa ujumla kuelendelea kuliombea Taifa hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba 2025.

Askofu Joseph Mlola amesema hayo wakati wa misa iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Maria mama wa Mungu Kibondo iliyoambatana na harambe ya ujenzi wa kanisa kubwa la kisasa parokiani hapo.

Muonekano wa bango la Kanisa la Parokia ya Mtakatifu Maria Mama wa Mungu, Picha na Tryphone Odace

Amesema kumekuwa matukio mengi kwenye jamii ambayo yanakatisha tama jambo ambalo linahatarisha amani na utulivu wa jamii na taifa kwa ujumla.

Sauti ya Askofu wa Jimbo katoliki la Kigoma Muhashamu askofu Joseph Roman Mlola

Katika harambe hiyo, Mgeni rasmi alikuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Reli Nchini TRC, Masanja Kadogosa amesema taifa liko katika kipindi cha uchaguzi na hivyo jamii haina budi kuhubiri amani kwa ajili ya kizazi kijacho.

Sauti ya Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Reli Nchini TRC, Masanja Kadogosa

Aidha katika harambe hiyo iliyoendeshwa na Mkurugenzi wa TRC Masanja Kadogosa zaidi ya shilingi milioni mia mbili hamsini zimepatikana ili kuendelea na ujenzi wa kanisa hilo.

Baadhi ya waumini wakatoliki Parokia ya Mtakatifu Maria mama wa Mungu Kibondo wamesema suala la amanai ni muhimu huku wakipongeza harambe hiyo kwani itasaidia kuongeza sehemu ya kusalia.