Joy FM

Madiwani wapitisha bajeti ya shilingi bilioni 68.3 Geita

31 January 2025, 12:11

Madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Geita mkoani Geita, Picha na Samwel Masunzu

Madiwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Geita wamesema bajeti hiyo itaenda kusaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi

Na Samwel Masunzu – Geita

Baraza la madiwani la halmashauri ya manispaa ya Geita mkoani Geita limepitisha rasmu ya makadirio ya bajeti ya kiasi cha shilingi bilioni 68.3 kwa mwaka wa fedha wa 2025/26

Bajeti hiyo imepitishwa kupitia kikao cha baraza hilo ambacho kimefanyika eneo la uwekeza EPZA Bombambili mjini Geita

Madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Geita mkoani Geita, Picha na Samwel Masunzu

Mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Geita bw. Yefred Myenzi amesema bajeti hiyo ni ongezeko la asilimia 13.2 ya bajeti ya mwaka 2024/25 na watahakikisha wanadhibiti ukwepaji wa ulipaji wa kodi kupitia vyanzo vya mapato  vilivyokuwepo na vile vilivyoongezeka.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Geita Yefred Myenzi

Kwa upande wake kaimu mstahiki meya wa manispaa ya Geita Elias Ngole amesema bajeti hiyo itasaidia kuendelea kuongeza ukarabati wa miundombinu ikiwemo barabara na kufungua miradi mipya ya halmashauri.

Sauti ya kaimu mstahiki meya wa manispaa ya Geita Elias Ngole
Kaimu mstahiki meya wa manispaa ya Geita Elias Ngole, Picha na Samwel Masunzu