Joy FM

Tulia Usilie yatoa kadi za bima za afya kwa wanafunzi wenye ulemavu

4 June 2025, 15:32

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kabanga Mazoezi katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu kwenye picha baada ya kupewa kadi za bima, Picha na Hagai Ruyagila

Wanafunzi wenye ulemavu katika shule ya Kabanga mazoezi wapatiwa msaada wa bima za afya ili kuwasaidia kupata matibabu.

Na Hagai Ruyagila

Katika kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya afya nchini, Taasisi ya Usilie Tena yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam, imetoa msaada wa kadi za bima ya afya kwa baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Kabanga Mazoezi, iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu, mkoani Kigoma.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Taasisi ya Usilie Tena, Bi. Egra Kamugisha, amesema kutokana na hali duni na kushindwa kumudu gharama ya bima ya afya imepelekea taasisi hiyo kufanya hivyo maana afya bora ni msingi imara wa maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Usilie Tena, Bi. Egra Kamugisha, Picha na Hagai Ruyagila

Aidha Bi. Kamugisha amesema taasisi yake itaendelea kushirikiana na jamii pamoja na wadau mbalimbali katika kuboresha sekta ya afya, hasa kwa makundi yenye uhitaji mkubwa kama wanafunzi wa shule za msingi mijini na vijijini.

Sauti ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Usilie Tena, Bi. Egra Kamugisha

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kabanga Mazoezi, Bi. Happiness Boyi, licha ya kuishukuru taasisi hiyo kwa msaada huo ametoa wito kwa wadau mbali mbali wa maendeleo kuendelea kuisaidia jamii isiyokuwa na uwezo.

Sauti ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kabanga Mazoezi, Bi. Happiness Boyi
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kabanga Mazoezi katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu kwenye picha baada ya kupewa kadi za bima, Picha na Hagai Ruyagila

Naye Timotheo Mapengo, mmoja wa wanafunzi walionufaika na msaada huo, ameilishukuru taasisi ya Usilie Tena kwa moyo wao wa huruma na mchango wa kuboresha maisha ya wanafunzi.

Sauti ya imotheo Mapengo, mmoja wa wanafunzi walionufaika na msaada huo

Msaada huo sehemu ya juhudi endelevu za taasisi hiyo katika kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata haki ya msingi ya huduma za afya bora.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Usilie Tena, Bi. Egra Kamugisha, Picha na Hagai Ruyagila