Joy FM

Milioni 460 zajenga nyumba 4 za watumishi wa afya Kasulu

19 September 2024, 13:39

Muonekano wa nyumba za watumishi wa afya katika halmashauri ya wilaya kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Serikali imeesema itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa watumishi wa afya kwa kuwajengea nyumba za kuishi ili waweze kutoa huduma kwa wananchi wakiwa karibu na maeneo yao ya kazi.

Na Hagai Ruyagila – Kasulu

Jumla ya shilingi milioni 460  zimetumika katika ujenzi wa nyumba 4 za wahudumu wa afya katika hospitali ya halmashauri ya  wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kwa mapato ya ndani.

Akitoa taarifa  ya ujenzi wa nyumba hizo za watumishi wa sekta ya afya, Mhandisi wa mradi huo kutoka halmashauri ya wilaya ya Kasulu Julius Shirawi ameeleza manufaa ya mradi huo ni kuboresha  na kusogeza huduma Bora za afya Kwa jamii.

Sauti ya Mhandisi wa mradi huo kutoka halmashauri ya wilaya ya Kasulu Julius Shirawi

Kwa upande wake, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru taifa mwaka 2024 Godfrey Mnzava ameipongeza halmashauri hiyo Kwa ujenzi Bora wa nyumba hizo za watumishi Kwa mapato ya ndani huku akiwasisitiza watumishi na kuzitunza nyumba hizo.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Godfrey Mnzava akiwa tayari kuzindua mradi wa nyumba za watumishi Kasulu Dc
Sauti ya Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru taifa mwaka 2024 Godfrey Mnzava

Naye Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu Dr. Semistatus Mashimba amesema ujenzi wa nyumba hizo ni utekelezaji wa maagizo ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha watumishi wa idara ya afya wanakata katika mazingira Bora.

Julia Shirawi akisoma taarifa ya mradi, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu Dr. Semistatus Mashimba

Nao baadhi ya wahudumu wa afya katika halmashauri hiyo wanaotumia nyumba hizo wameipongeza serikali Kwa kuwajengea nyumba karibu kwani awali walikuwa wanakaa mbali na eneo wanapotolea huduma.

Sauti ya baadhi ya wahudumu wa afya katika halmashauri hiyo wanaotumia nyumba hizo

 Mwenge wa uhuru mwaka 2024 umebebwa na kaulimbiu isemayo tunza mazingira na shiriki uchaguzi wa serikali za mitaa Kwa ujenzi wa taifa endelevu.