Zenj FM

Mwani wawalisha, bei yawaumiza, wanawake wa kisiwa cha Uzi wasimulia changamoto zao

8 August 2026, 13:16

Baadhi ya wanawake wakulima wa mwani Uzi Tunguu Zanzibar.

Karibu msikilizaji wa 96.9 zenj fm redio  tunakukaribisha tena katika sehemu hii maalum ya makala yetu inayogusa maisha ya wananchi na changamoto zinazowakabili katika shughuli zao za kila siku.

Leo tunakuletea simulizi kutoka kwa wakulima wa mwani visiwani Zanzibar, ambao wameeleza kusikitishwa na athari zinazotokana na mabadiliko ya tabianchi, hali ambayo imekuwa ikikwamisha shughuli zao za kilimo cha zao hilo la biashara.

Mwani.

Wakulima hao wanasema, pamoja na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, bei ya mwani isiyoridhisha imekuwa ikiongeza ugumu katika maisha yao, huku juhudi zao za kulima na kuzalisha zao hilo zikiwa hazitoshelezi kukidhi mahitaji yao ya kila siku.

Sauti ya Ivan Mapunda.