Zenj FM

Wagombea 5 wa urais Zanzibar wakamilisha masharti, warejesha fomu ZEC

9 September 2025, 7:53 pm

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe.Jaji George J. Kazi akipokea fomu za uteuzi kutoka kwa Mgombea Kiti cha Urais kupitia tiketi ya Chama cha ADA-TADEA .Juma Ali Khatib katika hafla ya urejeshaji wa fomu ya Uteuzi Ugombea Kiti cha Urais 2025.

Na Mary Julius

Wagombea watano wa nafasi ya Urais wa Zanzibar wamerejesha fomu zao kwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) baada ya kukamilisha masharti yote ya kisheria, ikiwemo kupata wadhamini wasiopungua 1,000 kutoka katika mikoa yote mitano ya Zanzibar.
Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu yake Mgombea wa Chama cha MAKINI, Ameir Hassan Ameir, ameahidi kufuata nyayo za Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Mzee Abeid Amani Karume, kwa kuhakikisha analeta maendeleo kwa wananchi wa Zanzibar.

Sauti ya Mgombea wa Chama cha MAKINI, Ameir Hassan Ameir,

Kwa upande wake, Mgombea wa chama cha ADA-TADEA, Juma Ali Khatib, amesisitiza kuwa uamuzi wa chama chake kumuunga mkono Mgombea wa CCM, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, si wa mtu binafsi bali ni azimio la pamoja la chama.

Sauti ya Mgombea wa chama cha ADA-TADEA, Juma Ali Khatib.

Hadi sasa, wagombea watano kati ya 17 waliopanga kugombea wamesharejesha fomu kwa ZEC.