Zenj FM

Taasisi za kiraia,Pemba zamwaga neema kwa wananchi

19 March 2024, 4:30 pm

Baadhi ya sadaka ambazo zimegaiwa kwa wananchi.

Na Is-haka Mohammed.

Meya wa Manispaa ya Chake Chake Abdalla Hamad Abdalla amesema kazi za utoaji wa misaada na sadaka zinazofanywa na taasisi mbali mbali za kiraia zinaisaidia serikali kutatua changamoto zilizopo katika jamii.

Meya ameyasema hayo katika hafla ya  kukabidhi sadaka kwa ajili ya futari kwa wananchi wasiojiweza na wenye uhitaji zilizotolewa na Taasisi ya Tawakal Foundation Iftar kwa kushirikiana na Taasisi ya Takrima huko Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.

Amesema serikali imekuwa ikifarijika kuona taasisi hizo zimekuwa zikiisaidia kutatua changamoto mbali za wananchi.

Sauti ya Meya wa Manispaa ya Chake Chake Abdalla Hamad Abdalla.

Kwa upande wake Katibu wa Taasisi ya Tawakal Faundation Salma Abdalla Hemed ameomba taasisi kuendelea kutoa sadaka zao za Ramadhani kwani kuna uhitaji  katika maeneo mbali mbali.

Sauti ya Katibu wa Taasisi ya Tawakal Faundation Salma Abdalla Hemed

Nao baadhi ya wananchi waliopatiwa sadaka hizo wametoa shukrani zao kwa taasisi hiyo na kuwaombea dua wale waliochanga sadaka hizo hadi kuwafikia wao.

Sauti ya wananchi waliopokea msaada.

Miongoni mwa sadaka zilizotolewa na pamoja na Mchele, Sukari, Maharage, Tambi, Kanga, Mabaibui na Viatu ambapo jumla ya waislamu 85 wa kijiji hicho wamepatiwa sadaka hiyo.