Zenj FM

Bandari Pemba yakusanya zaidi ya bilion 2

14 August 2023, 1:54 pm

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Dr. Khalid Salim Moh`d (watatu kutoka kulia)akiongozana na wajumbe wa  Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi ilipotembelea bandari ya Mkoani Pemba.

Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar imetembelea  bandari ya Mkoani Pemba na kushuhudia madadiliko katika bandari hiyo ikiwemo  katika njia ya kupitia abiria ambapo sasa abiria wanaweza kupita bila ya kupigwa na jua au mvua inaponyesha.

Na Is-haka Mohammed Pemba

Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi imepongeza Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi kwa juhudi inazozichukua katika kuimarisha huduma za usafiri Nchini.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti  ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mwanaisha Khamis Juma mara ametoa pongezi hizo mara baada ya kupokea ripoti ya wizara hiyo huko Mkoani .

Amesema Wizara ya Ujenzi imekuwa  ikifanya maborosho katika kuhakikisha huduma za usafiri wa bahari na nchi kavu kuona zinaimarika.

Sauti ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti   Mwanaisha Khamis Juma.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Dr Khalid Salum Mohd amesema katika kipindi cha mwaka 2022/23 Wizara hiyo imekadiria  kukusanya jumla ya shilingi bilioni mbili milioni miasaba na sabiini na saba katika bandari ya Pemba, kupitia Vyanzo mbali mbali Vya mapato kwenya bandari hiyo.

Aidha Dr Khalid amesema Wizara imejipanga kufanya ukarabati wa miundombinu katika maeno ya bandari ili kuona huduma hiyo inakuwa yenye ubora.

Sauti ya Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Dr Khalid Salum Mohd.