Pambazuko FM Radio

Polisi yamulika Matrekta Mlimba Kuzuia ajali

29 July 2026, 07:43

Mheshimiwa Diwani Msumali akitoa neno kwa washiriki wa mafunzo – picha na: WP9079 Mary

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro kupitia kitengo cha usalama barabarani limeendeleza kampeni ya kutoa elimu kwa wamiliki na madereva wa matrekta na power tiller wilayani Mlimba ili kumaliza kabisa tatizo la ajali za barabarani.

Na: Isidory Mtunda

Jeshi la polisi wilayani mkoa wa Morogoro kupitia kitengo chake cha usalama barabarani limeendelea na kampeni ya kutoa elimu kwa wamiliki na madereva wa matrekta na Power tiller katika halmashauri ya wilaya ya Mlimba baada ya kukamilisha zoezi hilo katika halmashauri ya mji wa Ifakara.

DTO Kasongwa katika moja ya mikutano ya mafunzo

Akizungumza na wamiliki na madereva wa vyombo hivyo wa tarafa ya Mbingu, DTO Blandina Kasongwa amesema lengo la zoezi hilo ni kumaliza tatizo la ajali barabarani na sio kupunguza tu.

Sauti ta DTO Kasongwa

Naye Mkuu wa Kituo cha Polisi Mbingu, ASP Bertha Matiku, amewaasa wamiliki wa vyombo hivyo kuhakikisha wanaajiri madereva wanaokidhi vigezo na kukagua mizigo inayobebwa ili kuzuia hatari zinazoweza kujitokeza

Sauti ya mkuu wa kituo cha Polisi Mbingu – ASP Matiku

Kwa upande wao, washiriki wa mafunzo hayo wamemuomba DTO na timu yake kupeleka mafunzo hayo katika tarafa hiyo ili madereva wengi waweze kushiriki na hatimaye kupata leseni.

Wamiliki na madereva wa Trekta na Power tiller wakimsikiliza mkaguzi wa magari – SGT Rjabu picha na: WP9079 Mary
Sauti za wananchi wakiomba wapatiwe mafunzo ya udereva

Akijibu maombi ya wananchi hao, DTO Kasongwa amewashauri wale wote walio tayari kushiriki mafunzo hayo kujiorodheshe majina yao kisha kuwakabidhi kwa mkuu wa kituo au Diwani wa kata hiyo, Mheshimiwa Joseph Chrispin Msumaly, kwa ajili ya utekelezaji zaidi.

Sauti ya DTO Kasongwa