Pambazuko FM Radio
Pambazuko FM Radio
13 May 2026, 20:18

Wananchi wameiomba serikali kukarabati barabara hiyo haraka ili kuboresha mawasiliano na shughuli za kiuchumi.
Na Katalina Liombechi
Wananchi wa Kata ya Kibaoni katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara wameiomba serikali kutatua haraka ubovu wa barabara ya kuvuka reli kuelekea Uwanja wa Ndege, inayounganisha vitongoji vya Uwanja wa Ndege, Mji Mpya, Kilolelo, Kilama A na Kilama B.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Uwanja wa Ndege, Jeremiah Machibya, amesema hali hiyo imekuwa ikisababisha usumbufu mkubwa wa usafiri na usafirishaji wa mazao, hasa wakati huu mvua na kwamba magari kupita kwa shida, jambo linaloathiri biashara, wanafunzi na shughuli za kilimo.

Hata hivyo utakumbuka hivi Karibuni Mbunge wa Jimbo la Kilombero akiwa bungeni Jijini Dodoma alifikisha kilio hichio kwa Naibu Waziri wa TAMISEMI akihoji nini mpango wa dharura wa serikali kutatua changamoto hiyo hasa wakati huu wa mavuno.
Kuhusiana na jambo hilo katika Majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI Dkt.Festo Dugange amesema serikali inatambua shughuli ya kilimo na uhitaji wa suluhu ya barabara katika eneo la Ifakara na kwamba tayari kupitia kwa meneja wa TARURA Wilaya ya Kilombero na Mkoa wa Morogoro wameshafanya tathimini ya mahitaji ya matengenezo ya dharura,huku akiisisitiza TARURA Kufanya matengenezo maeneo waliyo na uwezo nayo ili kurahisisha wananchi kupitisha mazao yao kwa wakati huu,wakati serikali ikiendelea na mkakati wa kuja na suluhu ya kudumu.
