Pambazuko FM Radio

Wilaya tatu Morogoro zanufaika na elimu ya msaada wa kisheria

4 October 2023, 12:12 am

wananchi wakifuatilia mafundisho kutoka kwa mwezeshaji wa Morogoro Paralegal Center – Picha Isidory

Kituo cha msaada wa kisheria Morogoro Paralegal Center(MPLC), katika ziara ya uhamasishaji (outreach) kimebaini changamoto za kisheria kwa wakazi wilaya za Kilombero, Malinyi na Ulanga, ambao wanakabiliwa na migogoro ya ardhi, ndoa na mirathi

Na; Isidory Matandula

Wanasheria kutoka Kituo cha Msaada wa Kisheria Morogoro, wamebaini kuwa, wananchi wengi wanakabiliwa na changamoto za migogoro ya ardhi,  mirathi na ndoa.

kulia ni mwanasheria Recho Siwiti kusho ni mwananchi akipata msaada wa kishria – picha – Isidory

Hayo yamebainishwa na Recho Siwiti, alipohojiwa na Redio Pambazuko, akiwa katika kijiji cha Mbuyuni, wilaya ya Ulanga, kutaka kujua changamoto walizoibua zaidi katika mikutano ya uhamasishaji kwa wananchi.

Sauti ya Mwanasheria Recho Siwiti

Nao wananchi waliofikiwa na elimu hiyo, Selina Muhogo na Salma Bilauli wakazi wa kijiji cha Mbuyuni wilaya ya Ulanga, wamekiri kunufaika na mikutano hiyo, katika masuala ya sheria ya ardhi na mirathi.

Sauti za wananchi

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Mbuyuni, Musa Nyimbe amekipongeza kituo cha msaada wa Kisheria Morogoro kwa mpango huo wa kutoa elimu kwa kuzunguka kwenye vijiji, umesaidia jamii juu ya masuala ya sheria, hasa yanayohusu migogoro ya ardhi na Mirathi.

Sauti ya mwenyekiti Musa Nyimbe

Mikutano hiyo imefanyika katika wilaya za Kilombero, Malinyi na Ulanga yenye lengo la kuwawezesha wanawake kiuchumi na kutambua haki zao, chini ya mradi wa POWER, unaofadhiliwa na shirika la The Aga Khan Foundation.