Pambazuko FM Radio

Ajenda ya no reforms no election yatua Bonde la Kilombero

6 June 2025, 14:57

Picha ya wananchi waliohudhuria mkutano wa Chadema Kata ya Minepa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga(Picha na Elias Maganga)

Chadema tumesema yafanyike marekebisho ya sheria ndio tuingie kwenye uchaguzi 2025

Na Elias Maganga

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)kinaendelea na ziara yake Nchi nzima ya kuhamasisha Agenda ya kutoshiriki uchaguzi mkuu kama hakutakuwa na marekebisho makubwa ya mifumo na sheria za uchaguzi.

Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati akiwahutubia wananchi June 5,2025 wa Halmashauri ya Mlimba kata ya Igima,ulanga kata ya Minepa na Halmashauri ya Mji wa Ifakara Kata ya Ifakara Makamu mwenyekiti wa Chama hicho John Heche amesema wanachokitaka wao kufanyike  marekebisho ya sheria ili  washiriki uchaguzi mkuu wa2025.

Picha ya John Heche Makamu mwenyekiti Chadema Taifa(Picha na Elias Maganga)
Sauti ya John Heche Makamu mwenyekiti Chadema Taifa

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chedema Taifa Bi Rose Maimba amelaani utekaji na ameiomba jamii  kushirikiana  kulikemea .

Sauti ya Rose Maimba Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chedema Taifa