Pambazuko FM Radio

Polisi yakagua magari hospitali Mtakatifu Fransisko

14 August 2026, 14:41

Team ya DTO na watumishi wa Hospitali ya Mt. Fransisko – picha na Jacline Raphael

Kuelekea wiki ya nenda kwa usalama, Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Kilombero limefanya ukaguzi wa magari ya Hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mtakatifu Fransisko pamoja na magari ya watumishi, kwa lengo la kubaini kasoro na kuimarisha usalama wa wagonjwa, watumishi na watumiaji wengine wa barabara.

Na: Isidory Mtunda

Kuelekea wiki ya nenda kwa usalama, DTO wilaya ya Kilombero, ASP Blandina Kasongwa ameendesha zoezi la ukaguzi wa magari ya Hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mtakatifu Fransisko na watumishi, kwa mwaliko wa mkurugenzi wa Hospitali hiyo ndugu Solanus Fusi.

ASP Kasongwa katika mahojiano mwandishi wa Pambazuko radio – picha na Jacline Raphael

Akizungumza na Pambazuko radio, ASP Kasongwa amesema zoezi hilo wanaangalia mifumo yote saba ya gari ili kuona iwapo haina kasoro na ameweka bayana kuwa mmiliki wa gari anawajibika kulipia STICER ya Nenda kwa usalama kulingana na aina ya chombo.

Sauti ya ASP Kasongwa

Naye afisa utawala wa Hospitali hiyo bwana Ezekiel Joachim kwa niaba ya mkurugenzi, ameipongeza timu ya usalama barabarani wilaya ya Kilombero kwa kuendesha zoezi hilo kituoni hapo, kwani kwa kufanya hivyo kunaokoa muda wa madaktari na wauguzi kusitisha huduma kwa wagonjwa kwenda kushughulikia ukaguzi wa magari.

Sauti ya Ezekiel Joachim

Kwa niaba ya wafanyakazi wa hospitali hiyo, Dkt Godfrey Ligomba ameishukuru timu ya DTO kuwafuata eneo lao la kazi, kitendo hicho kimewakolea muda na amemshukuru mkurugenzi wake kwa kuratibu zoezi hilo.

Sauti ya Dkt Ligomba