Pambazuko FM Radio

Ikwambi waishukuru serikali kwa kupata umeme

2 September 2026, 14:02

Wananchi wa Kitongoji cha Ikwambi, Kijiji cha Sululu, Kata ya Signal wilayani Kilombero,wakishangilia baada ya kuwashwa umeme kwa mara ya kwanza (Picha na Kuruthum Mkata)

“Tunaishukuru Serikali kutufikishia umeme katika kitongoji chetu itatusaidia kukuza biashara, viwanda vidogo na shughuli za ujasiriamali.”-Wananchi Ikwambi

Na Kuruthum Mkata.

Wananchi wa Kitongoji cha Ikwambi, Kijiji cha Sululu, Kata ya Signal wilayani Kilombero, wameishukuru Serikali kwa kuwafikishia huduma ya umeme wakisema itasaidia kukuza biashara, viwanda vidogo na shughuli za ujasiriamali.

Wamamchi wa Kitongoji cha Ikwambi wakishuhudia zoezi la uwashaji wa umeme(Picha na Kuruthum Mkata).
Sauti za baadhi ya wananchi wa Ikwambi

Akizindua huduma hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya amewataka wananchi kutumia fursa ya umeme kuanzisha miradi ya uzalishaji na viwanda vidogo vitakavyoongeza ajira kwa vijana na kukuza uchumi wa eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya aliyeshika maiki(Picha na Kuruthum Mkata)
Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Wakili Dunstan Kyobya

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Bw. Said Majaliwa, amehimiza wananchi kutumia umeme kwa shughuli za uzalishaji na kuchangamkia mikopo ya halmashauri ili kuendeleza miradi ya maendeleo.

Sauti ya Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Bw. Said Majaliwa

Naye Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kusini Eng Hassani Sesala amewataka wananchi kutunza miundombinu ya umeme na kuitumia huduma hiyo kujiongezea kipato kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kusini Eng Hassani Sesala (Picha na Kuruthum Mkata)
Sauti ya Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kusini Eng Hassani Sesala