Pambazuko FM Radio
Pambazuko FM Radio
23 June 2026, 19:54

Inaelezwa kuwa udhibiti wa magonjwa ni njia muhimu ya kuongeza tija na kupunguza hasara kwa wafugaji
Na Henry Bernad Mwakifuna
Dokta Khamis Nyoni, Mkufunzi kutoka Wakala wa Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Morogoro, amesema kuwa ufugaji bora unaweza kumwezesha mfugaji kupata faida kubwa.
Ameeleza kuwa mbuzi anaweza kuuzwa kwa hadi shilingi milioni 9, na wiki hii ng’ombe mmoja ameuzwa kwa shilingi milioni 15 katika eneo la Ubena Zomozi, Mkiani Morogoro.
Akifafanua zaidi, Dokta Nyoni amesema kuwa matumizi ya vinasaba husaidia kuzalisha mifugo yenye misuli mingi na uzito mkubwa, huku ng’ombe wa maziwa wakitoa maziwa kwa wingi.
Aidha, amesisitiza kuwa udhibiti wa magonjwa ni nguzo muhimu ya kuongeza tija na kupunguza hasara kwa wafugaji.
