Pangani FM
Pangani FM
22 June 2026, 12:53

Na Saa Zumo
Katika miaka ya nyuma, baadhi ya wanafunzi wa kike Wilayani Pangani mkoani Tanga walikumbwa na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikichangia kushuka kwa hamasa ya elimu na ufaulu katika masomo yao.
Baada ya Serikali kuweka mikakati ya kuboresha miundombinu ya shule za sekondari kupitia ujenzi wa madarasa, maabara, mabweni, hosteli, nyumba za walimu, shule mpya za amali na kuhakikisha wanafunzi wanapata vifaa vya kujifunzia ikiwemo vitabu na vifaa vya maabara.
Hamasa ya elimu kwa wasichana imeongezeka na sasa wanafanya vizuri hususani katika masomo ya Sayansi.