Pangani FM

Elimu yahitajika kukomesha unyanyapaa kwa wagonjwa wa afya ya akili

10 October 2023, 2:50 pm

Picha kutoka mtandaoni

“Magonjwa ya afya ya akili yanatibika iwapo utabaini mapema na kuanza matibabu

Na Mwandishi wetu

Kukosekana kwa elimu ya kutosha kwenye jamii juu ya magonjwa ya afya ya akili kumechangia unyanyapaa kwa watu wanaougua magonjwa hayo.

Hayo yamesemwa na mwanasaikologia Anastazia Nturu kutoka kituo cha Nobal Health kilichopo jijini Dar es Salaam wakati akiongea na Pangani FM kupitia kipindi cha Asubuhi ya leo ikiwa dunia inaadhimisha siku ya afya ya akili.

Sauti ya Anastazia Nturu

Amezitajia dalili za ugonjwa ikiwa ni pamoja na mtu kushindwa kutekeleza majumu yake ipasavyo na kuonesha hali ya wasiwasi

Sauti ya Anastazia Nturu

Kwa upande wake mwanasaikolijia Alpha Kipanga kutoka kituo cha Nobal Health ameishauri jamii kuwa makini katika kutambua mabadiliko ya mtu mmoja mmoja na kubaini kama mtu ameathiriwa na ugonjwa huo ili aweze kupata matibabu mapema kwani ugonjwa huo unatibika katika hatua za awali.

Sauti ya Alpha Kipanga