Pangani FM

Wodi ya NIKU yapunguza Vifo vya watoto wachanga wilayani Pangani

11 May 2026, 12:27

Picha ya Wodi maalumu ya uangalizi wa watoto wachanga na watoto njiti (NIKU). Picha na Saa Zumo

“Kuanzishwa kwa wodi maalumu ya uangalizi wa watoto wachanga na watoto njiti (NIKU) katika Hospitali ya Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, umeongeza upatikanaji wa huduma za karibu na kwa wakati kwa watoto wanaohitaji uangalizi maalumu”

Na Saa Zumo

Hospitali ya Wilaya ya Pangani mkoani Tanga ni moja kati ya Hospitali Kongwe hapa nchini ina Zaidi ya miaka 60 na tangu kuanzishwa kwake haikuwepo Wodi maalumu ya uangalizi wa watoto wachanga na watoto njiti (NIKU) jambo lililochangia watoto wanaozaliwa na changamoto za Upumuaji, Manjano, Moyo, Watoto njiti na wa Magonjwa mengine walikuwa wakipewa Rufaa kuelekea hospitali ya mkoa wa Tanga Bombo jambo lilichangia vifo vya watoto hao ambao walikuwa wakitokea maeneo mbali mbali ya wilaya ya Pangani.

Jengo la hospitali kwaajili ya Kliniki ya Baba, Mama na Mtoto. picha na Saa Zumo

Kuanzishwa kwa wodi maalumu ya uangalizi wa watoto wachanga na watoto njiti (NIKU) katika Hospitali ya Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, umeongeza upatikanaji wa huduma za karibu na kwa wakati kwa watoto wanaohitaji uangalizi maalumu.

Huduma hizo zimechangia kuboresha afya za watoto wachanga na kupunguza vifo vinavyotokana na kuzaliwa njiti au matatizo yanayotokea mara baada ya kuzaliwa.

Mwandishi wetu Saa Zumo ameandaa makala ifuatayo Bonyeza hapa kusikiliza hapa