Pangani FM

Umuhimu wa somo la Tehama kwa wanafunzi nchini

23 April 2026, 12:11

Tarakilishi miongoni mwa vifaa muhimu katika mfumo wa TEHAMA: Picha na Mtandao

Na Rajabu Mrope

Somo la TEHAMA liliingizwa kwenye mtaala wa elimu nchini Tanzania mwaka 2008 ikiwa ni miaka mitatu tu tangu kubadilishwa kwa mtaala kutoka ule wenye kujikita kwenye nadharia na kuhamia kwenye ule wenye kujikita katika umahiri.

Somo hili limekuwa lifundishwa kwa shule za msingi huku likikosa vifaa vinavyotarajiwa ili kukidhi malengo ya somo hilo pamoja na hali ya sasa ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.

Pamoja na hayo ila bado kuna changamoto za ufundishaji wa somo hilo kutokana na kukosekana kwa vifaa kama kompyuta,tablets ili kurahisisha ufundishwaji wake.

Sikiliza makala hapa