Sibuka FM
Sibuka FM
27 July 2026, 13:47

“Kila mtu anahaki ya kupata huduma bora bila kujali itikadi zao ili kufikia malengo yake tumetengeneza miundombinu bora nchini kwa kila sekta”.
Na,Daniel Manyanga
Mkuu wa wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Simon Simalenga amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Bariadi kuanza mara moja ujenzi wa shule mpya ya sekondari Matongo, iliyopo kata ya Matongo wilayani hapo na kuhakikisha ifikapo mwezi Januari 2027 wanafunzi waanze kusoma katika shule hiyo.
Simalenga ametoa agizo hilo baada ya kufika katika kata hiyo na kukagua zoezi la uchimbaji wa msingi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa shule hiyo ambapo amesema ni muhimu ujenzi huo ukaanza kwa haraka kwa ajili ya kuwaondolea wanafunzi wa kata hiyo changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata masomo ya sekondari.
Khalid Mbwana na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Bariadi, amesema kuwa ujenzi wa shule hiyo utawasaidia kwa kiasi kikubwa wanafunzi wa vijiji vya Matongo na Salalia kuondokana na changamoto ya kutembea umbali mrefu pamoja na vishawishi hasa kwa wanafunzi wa kike.
Samson Katambi, Kimola Sayi na Masunga Keya ni baadhi ya wakazi wa kata ya Matongo wameishukuru serikali kwa ujenzi wa shule hiyo na kusema kuwa itaondoa changamoto ya wanafunzi kukatisha masomo yao kutokana na umbali wa shule.