Sibuka FM

Wananchi wa kijiji cha Zebeya Wamemshukuru Rais Samia kwa kutoa Fedha Zaidi ya Shilingi Bilioni 1.6

11 October 2022, 5:03 pm

  1. Wananchi  wa  kijiji   cha  Zebeya  kilichopo  Kata  ya  Senani  Wilayani  Maswa  Mkoani  Simiyu  Wamemshukuru    Rais  wa  Jamhuri  ya  Muungano  wa   Tanzania   Mh  Samia  Suruhu  Hasani  kwa  kutoa  Fedha  Zaidi  ya  Shilingi  Bilioni  1.6    kwa  Ajili  ya  Ujenzi  na  Ukarabati  wa   Bwawa  la  Maji  la  Zebeya  na  Ilambambasa…

Emmanuel  Sule  na   Elisha  Jackson  ni  Wakazi  wa  kata  ya  Senani  Wilayani  Maswa  Wamesema  kuwa   kukamilika  kwa  Ujenzi  wa  Bwawa  hilo  utasaidia  kuwaondolea  Adha   ya  Maji waliyokuwa  wanapata  Pamoja  na  Changamoto  ya  Unyweshaji   maji  mifugo  yao..

Akitoa  Maelezo  kwa  Kamati  ya  Ulinzi  na  Usalama ya  Wilaya  iliyotembelea  Ujenzi   huo, Kaimu Mkurugenzi  Bodi  ya  Maji  Bonde  la  Ziwa  Victoria   Ogoma   Nyamhanga  amesema  kuwa  ni  vyema  Wananchi  wakawa  na  Uelewa  na  Faida za  Bwawa  kwa  kuacha  Shughuli  za  Kibinadamu  katika  njia  zinazoingiza  maji  katika  Bwawa  hilo..

Amesema  kuwa  Shughuli  za  kibinadamu  ndio  zinafanya  Bwawa  lijae Matope   hali  inayopelekea   ghaarama  nyingne  kwa  Serikali  kwa  kuanza  kuondoa  Mchanga  na  Tope  hivyo  ni  vizuri  Wananchi  wakaacha  shughuli  za  kilimo  kando  kando  ya  Bwawa  ili  kuepusha  Uharibifu  huo.

Aidha  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mh,  Aswege  Kaminyoge  amesema   Serikali  ya  Wilaya   itawapa  Ushirikiano    watu  wa  Bonde  la  Ziwa  Victoria  kwa  kutoa  Elimu  kwa  Wananchi  juu  ya  Utunzaji  wa  Vyanzo  vya  Maji  huku  akiwaomba   Watu  wa   Bonde  kuweka  Mipaka  ya  Bwawa  ili wananchi  sehemu  ambazo  hazipaswi  kufanya  shughuli za  kilimo..

Naye  Mkandara   anayejenga  Bwawa  hilo    Mhandisi  Edward  Malale  amesema  kuwa  kazi  imeshaanza   na  wapo  kwenye  Hatua  ya  Ujenzi  wa  Tuta ambalo  limekuwa  likibomoka  mara  kwa  mara  huku  kazi  yote   inategemea  kukamilika  Mwezi   Novemba  mwaka  huu  2022,   Ambapo  Bwawa  hilo  litanufaisha  Wakazi  Zaidi  ya  Elfu  11  na  Mifugo  zaidi  ya  Elfu  3  kutoka  kijiji  cha  Zebeya..