Sibuka FM

Wilaya ya Maswa  yaja  na  mkakati  wa  uzalishaji  zao  la  pamba  msimu wa  2023/2024

9 September 2023, 6:50 pm

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Maisha Mtipa akifafanua Mikakati ya Wilaya katika Uzalishaji wa zao la Pamba Msimu Ujao.

Na Nicholaus Machunda

Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa,  Mkoani  Simiyu  imejipanga  kuja  na  Mbinu  na  Mikakati itakayoongeza  Uzalishaji  wa  zao  la  Pamba  kwa  Msimu  ujao.

Hayo  yamesemwa  na  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Ndugu  Maisha Mtipa  wakati  wa  Mafunzo  ya  Kuwajengea  Uelewa  Madiwani  wa  Halmashauri  ya  Maswa  kuhusu  Kilimo  cha  zao  la  Pamba.

Sauti ya DED Maswa Ndugu Maisha Mtipa

Akiwasilisha  Mada  juu  ya  Sheria  zinazoongoza  kilimo  cha  Pamba, Mwanasheria  kutoka  Bodi  ya  Pamba  Tanzania  Bi, Elizabeth  Msuya  amesema  kuwa   kwa  Mjibu  wa  Kifungu  cha  Tano  cha  Sheria  ya  pamba, Bodi  inajukumu  la  kuishauri  Serikali juu  ya  kuleta  Maendeleo  katika Sekta  ya  Pamba.

Sauti ya Mwanasheria wa Bodi ya Pamba Tanzania Bi Elizabeth Msuya

           INSERT  02.  ELIZABETH  MSUYA- MWANASHERIA WA BODI

Aggrey  Mwanri   ni  Balozi  wa  Pamba  Nchi  Tanzania amesema  kuwa  ili  kuwe  na  Tija  katika  Uzalishaji   wa  zao  la Pamba  ni  vyema  Wakulima  wakaondokana  na  Kilimo  cha  Mazoea  ambacho  hakifuati  kanuni  kumi  za  Kilimo  cha  Zao  hilo.

Aliyekaa ni Balozi wa Pamba Tanzania Aggrey Mwanri
Sauti ya Balozi wa Pamba Tanzania Aggrey Mwanri

Kwa  Upande  wake   Mkuu  wa  Divisheni  ya  Kilimo, Mifugo  na  Uvuvi  Wilayani  hapa  Robert  Urassa  amesema  kuwa  kwa  msimu  wa  2023/ 2024  Wilaya  ya  Maswa  inatarajia  kulima Hekta  zaidi  ya  Elfu  Sitini  na  kuvuna  Tani  zaidi  ya  Elfu Sitini  za  Pamba   huku  akitaja   mikakati  ya  kufikia  malengo  hayo.

Sauti ya Robert Urassa – DAICO Maswa

Baadhi  ya  Madiwani  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  wameahidi  kushirikiana  na  Halmashauri katika  kutoa  Elimu  kwa  Wakulimu  na  wao   Kuanzisha  Mashamba Darasa  yatakayokuwa  mfano  kwa  Wakulima  kwenda  kujifunza.

Sauti za Baadhi ya Madiwani Halmashauri ya Maswa