Sibuka FM

DC Maswa Atoa Siku 14 Watendaji Kukabidhiana Ofisi

4 April 2024, 3:02 pm

Pichani Aliyesimama ni Mkuu wa wilaya ya Maswa ,Mhe Aswege Kaminyoge akizungumza na Wananchi wakati wa mkutano wa hadhara kijijini Bugalama picha na Nicholaus Machunda

Watendaji wote waliotajwa kula fedha za maendeleo zitokanazo na michango ya Wananchi ndani ya siku kumi na Nne warudishwe Ili kuja kujibu tuhuma na kufanya makabidhiano Mbele ya Serikali ya Kijiji.

Na, Daniel Manyanga

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mkoani  Simiyu  Aswege Kaminyoge  ametoa siku kumi na nne kwa Watendaji katika Kijiji na kata ya Bugalama waliowahi kufanya kazi hapo kurudishwa mara moja ili kuja kujibu tuhuma zinazowakabili  za utafunaji wa fedha za maendeleo zilizochangwa na Wananchi pamoja na kufanya makabidhiano mbele ya Serikali ya Kijiji.

Kaminyoge ametoa agizo hilo kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Maisha Mtipa Wakati wa Mkutano  ya  Hadhara wa kusikiliza kero mbalimbali za Wananchi na kuweza kuzitafutia utatuzi ili kuweza kuondoa kero kwa jamii na kuendelea kusimamia  dhana  ya  Utawala  Bora

Aswege Kaminyoge  amesema kuwa Watendaji wanaotajwa na Wananchi kutafuna fedha za maendeleo zinazotokana na michango ya Wananchi kijijini hapo lazima warudishwe mara moja ili kuja kujibu tuhuma hizo pamoja na kufanya makabidhiano mbele ya serikali ya kijiji hicho ili wananchi wapate nafasi ya kuhoji michango yao imefanya kazi gani huku Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Utumishi nao wakitakiwa kuwepo kwenye makabidhiano pamoja na mkutano huo.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa ,Aswege Kaminyoge akitoa siku kumi na Nne watendaji kurudishwa Ili kukabidhiana na kujibu tuhuma zinazowakabili.

Awali Robert Machiya mkazi wa kijiji cha Bugalama alipata nafasi ya kuwasilisha kero yake kwa mkuu wa wilaya hiyo ambapo alihoji ni sheria ipi inayompa mamlaka Mtendaji wa Kijiji au kata kutafuna fedha za maendeleo zinazotokana na michango ya Wananchi katika kijiji au Kata moja na kuhamishiwa kijiji/kata nyingine tena hata bila ya kuchukuliwa hatua zozote za kisheria.

Sauti za baadhi ya Wananchi wakitoa kero zao Mbele ya mkuu wa wilaya na Maswa wakati wa mkutano wa hadhara.