Sibuka FM

Jamii ya wafugaji, wadzabe wanufaika na mafunzo ya sheria ya ardhi

4 April 2024, 5:31 pm

Pichani:Anaeandika ni Samweli Kidima mshiriki wa mafunzo akiwa na washiriki wenzake kwenye mjadala wa pamoja.Picha na Alex Sayi

Jamii ya wafugaji na Wahadzabe wamenufaika na mafunzo ya Sheria ya Ardhi kwa lengo la kuzisaidia jamii hizo kujua  hatua za utatuzi wa migogoro kwenye maeneo yao.

Na,Alex Sayi

Shirika la DANMISSION kwa ushirikiano na kanisa la KKKT Jimbo la Bariadi Mjini Dayosisi ya kusini Mashariki ya Ziwa Victoria wameziwezesha jamii za kifugaji na jamii za waokota matunda  na wawindaji asilia(Hadzabe)kupata uelewa wa Sheria ya Ardhi ya mwaka (1999)

Hayo yamesemwa na mwanasheria kutoka Shirika la Pastoralists Indigenous Non-Governmental Organazation’sForum(PINGO’S FORUM)Saitoti Parmelo wakati wa wafunzo yaliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Sunga Kingdom Hotel Mkoani Simiyu.

Sauti ya Mwanasheria wa Pingo’sForum Saitoti Parmelo

Parmelo ameongeza kuwa lengo la mradi huo nikuzileta pamoja jamii za wafugaji ,wawindaji na  waokota matunda asilia ili kujadili changamoto zinazozikabili jamii hizo.

Sauti ya Mwanasheria wa Pingo’s Forum Saitoti Parmelo
Pichani:Mwanasheria wa Pingo’s Forum Saitoti Parmelo akiwa kwenye maandalizi ya uwasilishaji wa mada kwa washiriki.Picha na Alex Sayi.

Kwa upande wake Afisa Mipango,Miradi na Afya toka Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Martha Mwakisu amesema kuwa mradi  umelenga  kuziwezesha jamii hizi kuwa na uwezo wakujitegemea  kwenye utatuzi wa  migogoro pale  inapojitokeza.

Sauti ya Afisa Mipango,Miradi na Afya Bi,Martha Mwakisu
Pichani:Bi,Martha Mwakisu Afisa Mipango,Miradi na Afya akiwasilisha mada kwa washiriki wa mafunzo
Pichani:Bi,Martha Mwakisu Afisa Mipango,Miradi na Afya akiwasilisha mada kwa washiriki wa mafunzo.Picha na Alex Sayi.

Samson Salehe mshiriki wa mafunzo hayo amesema kuwa jamii ya Wahadzabe wamefurahi kupata fursa hiyo yakupata mafunzo hayo kwakuwa ni jamii ambayo inakabiliwa na changamoto yakupoteza asili yake.

Sauti ya Samson Salehe(Mhadzabe)